Skip to main content

Full text of "Biblia yenye vitabu vya Deuterokanoni habari njema: Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa"

See other formats


MWANZO 



Kuumbwa ulimwengu 

11 Hapo mwanzo, Mungu aliumba 
mbingu na dunia.« ^Dunia ilikuwa 
bila umbo na tupu. Giza lilikuwa lime- 
funika vilindi vya maji na roho ya 
Mungu ^ ilikuwa ikitanda juu ya maji. 

3 Mungu akasema, "Mwanga uwe," 
mwanga ukawa. ^ Mungu akauona mwa- 
nga kuwa ni mwema. Kisha Mungu 

8 Mungu akaliita anga "Mbingu." Ikawa 
jioni, ikawa asubuhi; siku ya pili. 

9 Mungu akasema, "Maji yaliyo chini 
ya mbingu na yakusanyike mahali pamo- 
ja, nchi kavu itokee." Ikawa hivyo. 
1® Mungu akapaita mahali pakavu "Nchi" 
na kusanyiko la maji akaliita "Bahari." 
Mungu akaona kuwa ni vyema. 

11 Kisha Mungu akasema, "Ardhi 
na ioteshe mimea: mimea izaayo mbe- 
gu, na miti izaayo matunda yenye 
mbegu." Ikawa hivyo. i^Basi, ardhi 
ikaotesha mimea izaayo mbegu kwa 
jinsi yake, na miti izaayo matunda yenye 
mbegu kwa jinsi yake. Mungu akaona 
kuwa ni vyema. "i^awa jioni, ikawa 
asubuhi; siku ya tatu. 

14 Mungu akasema, "Mianga na 
iweko angani, itenge mchana na usiku, 
ionyeshe nyakati, majira, siku na miaka, 
15 na ing'ae angani na kuiangazia dunia." 
Ikawa hivyo. i^Basi, Mungu akafanya 
mianga miwili mikubwa; ule mkubwa 
utawale mchana na ule mdogo utawale 
usiku; akafanya na nyota pia. ^^ Mungu 
akaiweka mianga hiyo angani iiangazie 
dunia, i^ipate kutawala mchana na 
usiku, na kuutenga mwanga na giza. 



akautenganisha mwanga na giza, ^ mwa- 
nga akauita "Mchana" na giza akaliita 
"Usiku." Ikawa jioni, ikawa asubuhi; 
siku ya kwanza. 

6 Mungu akasema, "Anga liwe kati- 
kati ya maji, liyatenge maji sehemu 
mbili." 7 Mungu akalifanya anga, akaya- 
tenga maji yaliyo juu ya anga na yale 
yaliyo chini ya anga hilo. Ikawa hivyo. 

Mungu akaona kuwa ni vyema. i* Ikawa 
jioni, ikawa asubuhi; siku ya nne. 

20 Mungu akasema, "Maji na yatoe 
makundi ya viumbe hai na ndege waru- 
ke angani." ^iBasi, Mungu akaumba 
wanyama wakubwa sana wa baharini na 
aina zote za viumbe vyote hai viendavyo 
na kujaa majini; akaumba na aina zote 
za ndege wote. Mungu akaona kuwa ni 
vyema. 22 Mungu akavibariki, akasema, 
"Zaeni, mwongezeke, myajaze maji ya 
bahari; nao ndege waongezeke katika 
nchi." 23 Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku 
ya tano. 

24 Mungu akasema, "Ardhi na itoe 
aina zote za viumbe hai, wanyama wa 
kufugwa, viumbe vitambaavyo na wa- 
nyama wa porini wa kila aina." Ikawa 
hivyo. 25 Basi, Mungu akafanya aina zote 
za wanyama wa porini, wanyama wa 
kufugwa, na viumbe vitambaavyo. Mu- 
ngu akaona kuwa ni vyema. 

26 Kisha Mungu akasema, "Tumfa- 
nye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; 
atawale samaki wa baharini, ndege wa 
angani, wanyama wa kufugwa, dunia 
yote na viumbe vyote vitambaavyo." 
27 Basi, Mungu akaumba mtu kwa nmno 
wake; naam, kwa mfano wake Mungu 



« 1:1 Hapo . . . dunia: au: Hapo mwanzo, Mungu alipoziumba mbingu na dunia, 2 dunia. 
* 1:2 roho ya Mungu: au: upepo mkubwa. 



MWANZO 1-2 



alimwumba. Aliwaumba mwanamume 
na mwanamke. zsMungu akawabariki na 
kuwaambia, "Zaeni mwongezeke, mkai- 
jaze nchi na kuimiliki; mwatawale sama- 
ki wa baharini, ndege wa angani, na kila 
kiumbe hai kitembeacho duniani." 

29 Kisha Mungu akasema, "Tazama, 
nawapeni kila mmea duniani uzaao 
mbegu, na kila mti uzaao matunda 
yenye mbegu; mbegu zao au matunda 
yao yatakuwa chakula chenu. ^oNao 
wanyama wote duniani, ndege wote wa 
angani, viumbe vyote vitambaavyo, naa- 
m, kila kiumbe chenye uhai, chakula 
chao kitakuwa majani yote ya mimea." 
Ikawa hivyo. ^i Mungu akaona kila kitu 
alichofanya kuwa ni chema kabisa. 
Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya sita. 

21 Hivyo ndiyyo mbingu na dunia 
zilivyokamilika pamoja na vitu vyo- 
te vilivyomo. 2 Siku ya saba Mungu 
akawa amemaliza kazi yake yote aliyo- 
fanya; siku hiyo ya saba Mungu akapu- 
mzika baada ya kazi yake yote aliyofa- 
nya. ^ Mungu akaibariki siku ya saba na 
kuitakasa, kwa kuwa siku hiyo Mungu 
alipumzika baada ya kazi yake yote ya 
kuumba. * Hivyo ndivyo mbingu na 
dunia zilivyoumbwa. 

Bustani ya Edeni 

Siku ile Mwenyezi-Mungu*^ alipoziu- 
mba mbingu na dunia, ^Hapakuwa na 
mimea juu ya nchi wala miti haikuwa 
imechipua kwani Mwenyezi-Mungu ha- 
kuwa ameinyeshea nchi mvua, wala 
hapakuwa na mtu wa kuilima. *Hata 
hivyo, maji yalitoka ardhini yakainywe- 
sha ardhi yote. ^Basi, Mwenyezi-Mungu 
akamwumba mwanamume kwa udongo, 
akampulizia puani pumzi ya uhai, na 
huyo mwanamume akawa kiumbe hai. 

8 Kisha Mwenyezi-Mungu akapanda 
bustani huko Edeni, upande wa masha- 
riki, na humo akamweka huyo mwana- 
mume aliyemwumba. 'Mwenyezi-Mu- 
ngu akaotesha kutoka ardhini kila aina 
ya miti mizuri izaayo matunda yafaayo 
kwa chakula. Katikati ya bustani hiyo 
kulikuwa na mti wa uhai na mti wa ujuzi 
wa mema na mabaya.'' 



10 Kulikuwa na mto huko Edeni 
uUotiririka maji na kuinywesha hiyo 
bustani; kutoka huko mto huo uligawa- 
nyika kuwa mito minne. "Jina la mto 
wa kwanza ni Pishoni; huo waizunguka 
nchi yote ya Hawila ambako kuna 
dhahabu. i^ohahabu ya nchi hiyo ni 
safi kabisa. Huko pia kuna marashi 
yaitwayo bedola na vito viitwavyo sho- 
hamu. i3jina la mto wa pili ni Gihoni; 
huo waizunguka nchi yote ya Kushi.« 
i*Jina la mto wa tatu ni Tigri,/ nao 
watiririkia upande wa mashariki wa 
nchi ya Ashuru; na jina la mto wa nne 
ni Eufrate. 

15 Basi, Mwenyezi-Mungu aka- 
mtwaa huyo mwanamume, akamweka 
katika bustani ya Edeni, ailime na 
kuitunza. i« Mwenyezi-Mungu alimwa- 
muru huyo mwanamume, "Waweza ku- 
la matunda ya mti wowote katika 
bustani; I'^lakini matunda ya mti wa 
ujuzi wa mema na mabaya, usile, maana 
siku utakapokula matunda ya mti huo, 
hakika utakufa." 

18 Kisha Mwenyezi-Mungu akase- 
ma, "Si vizuri huyu mwanamume kuwa 
peke yake. Nitamfanyia msaidizi wa 
kumfaa." ^'Basi, kutoka katika udongo, 
Mwenyezi-Mungu akaumba kila mnya- 
ma wa porini na kila ndege wa angani, 
halafu akamletea huyo mwanamume 
aone atawapa majina gani; na majina 
aliyowapa viumbe hao, yakawa ndiyo 
majina yao. 20 Basi, huyo mwanamume 
akawapa majina wanyama wote wa 
kufugwa, wanyama wa porini na ndege 
wote wa angani. Lakini hakupatikana 
msaidizi yeyote wa kumfaa. 

21 Basi, Mwenyezi-Mungu akamle- 
tea huyo mwanamume usingizi mzito, 
na alipokuwa usingizini, akatwaa ubavu 
wake mmoja na kupafunika mahali pale 
kwa nyama. 22 Na huo ubavu Mwenye- 
zi-Mungu alioutoa kwa yule mwanamu- 
me akaufanya kuwa mwanamke, aka- 
mleta kwa huyo mwanamume. ^sNdipo 
huyo mwanamume akasema, 

"Naam! Huyu ni mfupa kutoka 
mifupa yangu, 

na nyama kutoka nyama yangu. 



1:27-28 taz 5:1-2 

c I'A Mwenyezi-Mungu: katika makala ya Kiebrania ni Yahweh, jina takatifu la Mungu ambalo 

katika utamaduni wa Wayahudi halikutamkwa. 
^ 2:9 mti wa uhai: Ufu 2:7; 22:2,14; ujuzi wa mema na mabaya; tafsiri nyingine: ujuzi wa kila kitu 

(vilevile aya 17 na 3:5,22.) 
< 2:13 nchi yote ya Kushi: hufikiriwa na wengine kuwa Mesopotamia. Lakini baadhi wadhani ni 

sehemu ya kusini ya Misri (Sudani au Ethiopia.) 
/ 2:14 Tigri: Kiebrania: mto huo ni Hidekeli. 



MWANZO 2-3 



Huyu ataitwa 'Mwanamke',^ 
kwa sababu ametolewa katika 
mwanamume." 
24Ndiyo maana mwanamume humwa- 
cha baba yake na mama yake, akaamba- 
tana na mkewe, nao wawili huwa mwili 
mmoja. 

25 Huyo mwanamume na mkewe wo- 
te walikuwa uchi, lakini hawakuona haya. 

Uasi wa binadamu 

31 Nyoka alikuwa mwerevu kuliko 
wanyama wote wa porini waliou- 
mbwa na Mwenyezi-Mungu. Basi, nyoka 
akamwambia huyo mwanamke, "Ati 
Mungu alisema msile matunda ya mti 
wowote bustanini?" ^ Mwanamke aka- 
mjibu huyo nyoka, "Twaweza kula ma- 
tunda ya mti wowote bustanini; ^ lakini 
Mungu alisema, 'Msile matunda ya mti 
ulio katikati ya bustani, wala msiuguse, 
msije mkafa.'" ^ Nyoka akamwambia 
mwanamke, "Hamtakufa! * Mungu ali- 
sema hivyo kwa sababu anajua kwamba 
mkila matunda ya mti huo mtafumbuli- 
wa macho, nanyi mtakuwa kama Mu- 
ngu, mkijua mema na mabaya." 

6 Basi, mwanamke alipoona kuwa 
mti huo ni mzuri kwa chakula, wavutia 
macho, na kwamba wafaa kwa kupata 
hekima, akachuma tunda lake, akala, 
akampa na mumewe, naye pia akala. 
■'Mara macho yao yakafumbuliwa, wa- 
katambua kwamba wako uchi; hiyyo 
wakajishonea majani ya mtini, wakajifa- 
nyia mavazi ya kiunoni. 

SJioni, wakati wa kupunga upepo, 
huyo mwanamume na mkewe wakasikia 
hatua za Mwenyezi-Mungu akitembea 
bustanini, nao wakajificha kati ya miti ya 
bustani, Mwenyezi-Mungu asipate ku- 
waona. 'Lakini Mwenyezi-Mungu aka- 
mwita huyo mwanamume, "Uko wapi?" 
^•Naye akamjibu, "Nimesikia hatua zako 
bustanini, nikaogopa na kujificha, maana 
nilikuwa uchi." " Mwenyezi-Mungu aka- 
mwuliza, "Nani aliyekuambia kwamba 
uko uchi? Je, umekula tunda la mti 
nililokuamuru usile?" ^^Huyo mwana- 
mume akajibu, "Mwanamke uliyenipa 
akae pamoja nami ndiye aliyenipa tunda 
la mti huo, nami nikala." 

13 Hapo Mwenyezi-Mungu akamwu- 
liza huyo mwanamke, "Umefanya nini 
wewe? Mwanamke akamjibu, "Nyoka 
alinidanganya, nami nikala." 



Adhabu 

14 Kisha Mwenyezi-Mungu akamwa- 
mbia nyoka, 

"Kwa kuwa umefanya hivyo, 
umelaaniwa kuliko wanyama wote 

wa kufugwa, 
na kuliko wanyama wote wa 

porini. 
Kwa tumbo lako utatambaa, 
na kula mavumbi siku zote za 

maisha yako. 
1* Nitaweka uadui kati yako na 

huyo mwanamke, 
kati ya uzao wako na uzao wake; 
yeye atakiponda kichwa chako, 
nawe utamwuma kisigino chake." 

16 Kisha akamwambia mwanamke, 
"Nitakuzidishia uchungu wa kuzaa, 
kwa uchungu utazaa watoto; 
utakuwa na hamu na mumeo, 
naye atakutawala." 

17 Kisha akamwambia huyo mwana- 
mume, 

"Kwa kuwa wewe umemsikiliza 

mkeo, 
ukala matunda ya mti ambayo 

nilikuamuru usile; 
kwa hiyo, kwa kosa lako ardhi 

imelaaniwa. 
Kwa jasho utajipatia humo riziki 

yako, 
siku zote za maisha yako. 
18 Ardhi itakuzalia miiba na magugu, 
nawe itakubidi kula majani ya 
shambani. 
1' Kwa jasho lako utajipatia chakula, 
mpaka utakaporudi udongoni 

ulimotwaliwa; 
maana wewe ni mavumbi, na 

mavumbini utarudi." 
20 Adamu* akampa mkewe jina "Ha- 
wa",' kwani alikuwa mama wa binadamu 
wote 21 Mwenyezi-Mungu akawatengene- 
zea Adamu na mkewe mavazi ya ngozi, 
akawavika. 

Adamu na Hawa 
wanafukuzwa bustanini 

22 Kisha Mwenyezi-Mungu akasema, 
"Sasa, binadamu amekuwa kama nmioja 
wetu, anajua mema na mabaya. Lazima 
kumzuia kula lile tunda la mti wa uhai, 
kwani akilila ataishi milele!" ^agasj^ 
Mwenyezi-Mungu akamfukuza Adamu 
nje ya bustani ya Edeni, ili akailime ardhi 



g 2:23 Kiebrania: maneno mwanamume . . . mwanamke; "ishi, isha" yanafanana. 

^ 3:20 Adamu: Kiebrania maana yake ni "mtu". 

' 3:20 Hawa: Kiebrania lalingana na neno lenye maana "uhai". 



MWANZO 3-5 



ambamo alitwaliwa. 24 Alimfukuza nje, na 
loiweka mlinzi> upande wa masharud wa 
bustani ya Edeni na upanga wa moto 
uliogeuka huko na huko, kuilinda njia 
iendayo kwenye mti wa uhai. 



atalipizwa mara saba." Basi, Mwenyezi- 
Mungu akamtia Kaini alama ya tahadha- 
ri, ill yeyote atakayemwona asimwue. 
i^Kisha Kaini akaondoka mbele ya Mwe- 
nyezi-Mungu, akawa anaishi katika nchi 
ya Ncxii,' upande wa mashariki wa Edeni. 



The Bible with Deuterocanonicals in current Kiswahili 

An Interconfessional Translation published as 

BIBLIA 

Yenye Vitabu vya Deuterokanoni 

HABARI NJEMA 

Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa 

Published by 

The Bible Society of Kenya 

P.O. Box 72983 

NAIROBI, Kenya 

and 

The Bible Society of Tanzania 

P.O. Box 175 

DODOMA, Tanzania 

© The Bible Society of Kenya, 1995 
© The Bible Society of Tanzania, 1995 
Illustrations by Horace Knowles 
© The British and Foreign Bible Societ 
London, England, 1954, 1967, 1972. 

All Rights Reserved 

First Published 1995 



ISBN 9966 - 40 - 592 - 5 - CLDC053P - 40M 
ISBN 9966 - 40 - 593 - 3 - CLDC057P - 0.5M 
KISWAHILI BIBLE DC EDITION UBS-EPF 40.5M 199' 



BIBLIA 

Yenye Vitabu vya Deuterokanoni 
HABARI NJEMA 

TAFSIRI YA USHIRIKIANO WA MAKANISA 



VYAMA VYA BIBLIA 

KENYA NA TANZANIA 

NAIROBI : DODOMA 

Eunice V. Pike Library 

SUMMER INSTITUTE OF LINGUISTICS 
Dallas, Texas 

Given by: 

BIBLE TPANSLATION 

AND LITERACY: 
THE NBTO OF KENYA